Jeshi la polisi Mkoa wa Katavi linawasaka watu watatu kwa tuhuma za kumuuwa na kisha kumfukia aridhini Mbaya Lukondia (36) mkazi wa Kijiji cha Kabunde Kata ya Mamba Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi .
Kamanda wa jeshi la polisi wa Mkoa wakazi aliwataja watuhumiwa hao wanaotafutwa kuwa ni Ubakila Kidakira , Jimon Dogi (lala)na mtu mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Omary wote wakazi wa Kijiji cha Kabunde Kata ya Mamba Wilaya ya Mlele .
Kwa mujibu wa Kamanda Kidavashari ni kwamba kabla ya kifo hicho marehemu alitoweka nyumbani kwake mwezi Aprili mwaka huu na haikuweza kueleweka mahali alipo kuwa .
Alisema kwa kipindi chote hicho ndugu wa marehemu waliendelea kumtafuta hadi hapo june 19 alipogundulika akiwa amefukiwa aridhini huku mwili wake ukiwa umeharibika vibaya .
Alifafanua baada ya kufukuliwa kwa mwili huo wa marehemu na kufanyiwa uchunguzi ndipo ilipoonyesha kuwa marehemu aliuwawa kwa kupingwa na kitu kizito katika sehemu ya kichwani na ubavuni.
Alisema watuhumiwa hao wanadai baada ya kufanya mauwaji hayo walitoweka kijijini hapo na mpaka sasa hawaja fahamika mahali walipo kimbilia .
Alieleza wananchi wa kijiji hicho waliwatila mashaka ya kuhusika na tukio hilo baada ya mwili wa marehemu kupatika ukiwa umefukiwa aridhini na wao toka siku huyo walitoweka Kijijini .
Kamanda Kidavashari amesema jeshi la Polisi kwa kushirikiana na wananchi linaendelea kuwatafuta watuhuiwa hao watatu iliwakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Na Walter Mguluchuma -Mpanda Katavi
Social Plugin