Haya sasa!! CHAMA KIPYA CHA SIASA CHA ACT HATIMAYE CHAPATA USAJILI WA KUDUMU

Chama kilichovunja rekodi kwa kupata usajili wa kudumu miezi michache mara baada ya usajili wa muda; ACT-TANZANIA  jana ndio kimekabidhiwa cheti chake cha usajili wa kudumu rasmi na masajili wa vyama vya siasa mara baada ya kumalizika zoezi la usajili lililofanyika katika mikoa kumi iliyoteuliwa. 




kilifanikiwa kumaliza zoezi la uhakiki mara baada ya kuruka vihunzi vingi toka kwa wahafidhina na watu wasiopenda siasa za ushindani. 
 
Katika zoezi letu tumekumbana na vikwazo vingi ikiwa pamoja na uchomekaji wa wanachama fake waliotumwa kwaajili ya kazi ya kujifanya wako tayari kuhakikiwa lakini kwa lengo la kutojitokeza siku ya kuhakikiwa, jambo ambalo wahafidhina na maadui zetu walikuwa hawajui ni kuwa chama chetu kinapendwa na wananchi hivyo wengi walijitokeza kiasi cha kuziba mapengo ya mamluki ambao kwa makusudi hawajajitokeza siku ya kuhakikiwa. 


Pamoja na hayo tunatambua wanachama wetu waaminifu waliotaka kujitokeza lakini sababu zilizo nje ya uwezo wao zilipelekea washindwe kujitokeza siku ya kuhakikiwa. 

Karibu ACT-TANZANIA, wewe ndio mbadala wa CHADEMA na CCM. 
Mungu ibariki Tanzania.

Njano5.

Mwanachama.
0784845394

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments