MOYES KULA MAISHA BAADA YA KUTIMULIWA,SASA KULIPWA MAMILIONI YA FEDHA

Siku moja tu baada ya kutimuliwa kutoka kwenye kibarua cha kuifundisha klabu ya Manchester United imefahamika kwamba kocha David Moyes atalipwa fidia kutokana na klabu hiyo kuvunja mkataba wa miaka sita walioingia mwaka jana mwezi wa tano. 

David Moyes atalipwa fidia ya £5million baada ya kufukuzwa kazi na Manchester United – ikiwa ni kipengele cha makubaliano ya mkataba wake na klabu hiyo.


Katika mkataba wa Moyes na United kulikuwa na kipengele kinachoeleza ikiwa Manchester United ingefeli kufuzu kucheza Champions League msimu huu basi ikatokea United wakaamua kusitisha mkataba wake basi fidia isingezidi mshahara wake wa miezi 12 ambao ni £5million.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post