AFARIKI BAADA YA KUNG'ATWA NA NYOKA HUKO IRINGA


Mkazi wa kijiji cha Ilindi wilayani Kilolo Thomas Kilonge(42), amefariki dunia baada ya kung’atwa na nyoka.
 
Kaimu Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Iringa, Wankyo Nyigesa alisema tukio hilo limetokea juzi kijijini hapo na kumtaja aliyefariki kuwa ni mkulima wa kijiji cha Ilindi.
 

Hata hivyo alidai kuwa mazingira ya kung’atwa na mdudu huyo bado hayajajulikana na kwamba, jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi wake.
NA FRANK KIBIKI, IRINGA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post