Nzega Kwanuka!!!! WACHIMBAJI WADOGO WATAKIWA KUONDOKA MARA MOJA ENEO LA MACHIMBO YALIYOPO MWASHINA- NZEGA MKOANI TABORA

 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida wachimbaji wadogo kwenye machimbo ya Mwashina wilayani Nzega mkoani Tabora wametakiwa kuondoka eneo hilo kuanazia leo.Habari kutoka katika machimbo hayo zinasema kuwa tayari askari polisi wapo eneo hilo hata hivyo wachimbaji hao wanasema kuwa kuwafukuza kwenye machimbo hayo ni kuwanyima ajira na kwamba tayari walikuwa wametumia nguvu na fedha katika uchimbaji. 

Wakazi wa mji wa Nzega wamepokea kwa masikitiko makubwa kauli  ya Serikali ya kuwaondoa wachimbaji hao ambao walikuwa wanakuza uchumi wa mji huo na kuitaka Serikali kusitisha zoezi hilo kwa manufaa ya wakazi wa Nzega. 

                                 >>>>>>>>         HABARI ZAIDI BOFYA HAPA <<<<<<<<<

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post