Awali mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Nassoro Rufunga akifungua kikao cha kawaida cha 25 cha kamati ya Ushauri ya mkoa akimkaribisha katika kikao hicho waziri
wa nchi ofisi ya rais utawala bora inayohusika na masuala ya rushwa na maadili
ya viongozi George Mkuchika ili awasilishe mada juu ya utawala bora kwenye kikao cha kamati ya ushauri kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga.
|
Alisimama ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Shinyanga Khamis Mgeja akichangia mawili matatu katika kikao hicho ambapo aliipongeza serikali ya awamu ya nne kwa kusimamia mambo mbalimbali ya maendeleo likiwemo suala la kupiga vita rushwa huku akisema pamoja na jitihada za serikali kupiga vita adui Rushwa lakini kila mtu katika jamii ana wajibu wa kupiga vita rushwa.
|
Aliyesimama ni katibu msaidizi secretariati ya maadili ya viongozi wa umma kanda ya magharibi -Tabora Salvatory Kilasara akiwasilisha mada kuhusu sheria ya maadili ya viongozi wa umma na majukumu ya sekretariati ya maadili.
|