Hii kali!!! MWANAMKE AJIFUNGUA FARASI KANISANI



Waumini wa kanisa la ‘World liberation Ministry’ linalopatikana katika mji wa Sepele nchini Benin walikumbwa na mshangao baada ya mwanamke mmoja kujifungua farasi wakati wa misa ya maombi iliyofanyika katika kanisa hilo.


Hata hivyo wakati waandishi wa habari walipofika katika kanisa hilo, tayari farasi huyo alikuwa ameshakufa. Inasemekana kuwa mwanamke huyo ambaye jina lake bado halijajulikana, alianza kupiga kelele wakati wa maombi na kisha kuanza kutoa damu katika sehemu zake za siri kabla ya kujifungua farasi huyo. 

Msimamizi mkuu wa kanisa hilo, muinjilisti Silva Wealth alisema kuwa bado anashangazwa na kilichomtokea mwanamke huyo. Silva alisema kuwa wakati wa maombi alipata uono kuwa kuna mwanamke mwenye tatizo na kwamba kulikuwa kunakitu kinazuia... 

Silva aliendelea kusema kuwa maombi yalipopamba kasi, mwanamke huyo alianza kupiga kelele kisha damu zikaanza kumtoka halafu kikamtoka hicho kitu. 

“Siwezi kuelezea kitu hicho. Katika maombi yetu tumewahi kushuhudia watu wakitapika vitu mbalimbali, lakini sio kitu kama hiki.” Alisema muinjilisti Silva. 

Mara baada ya taarifa hizo kuzagaa mitaani, watu mbalimbali walianza kukimbilia katika kanisa hilo ili kuweza kushuhudia kwa macho yao.
Credit-Utamu specially

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post