 |
Katikati aliyevaa nguo nyeusi ni mkurugenzi
mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Mohamed Kiyungi -PICHA KUTOKA MAKTABA YA MALUNDE1 BLOG
Halmashauri
ya wilaya ya Shinyanga imedaiwa kuwalazimisha watumishi wake kukopa pikipiki
kwa lazima bila kujali hata kama mtumishi husika anayo yake binafsi hali ambayo
imezua maswali mengi kwa watumishi wake ambao wamedai huenda pikipiki hizo
zimepelekwa na kigogo mmoja ziuzike chap chap.
Wakizungumza
na waandishi wa habari mjini Shinyanga
kwa sharti la kutotajwa majina yao baadhi ya watumishi hao wamesema
wameshitushwa na kitendo cha mkurugenzi wa halmashauri hiyo ya wilaya, Mohamed Kiyungi
kulazimisha mikopo hiyo hata kama mtu hahitaji kukopa ambapo agizo hilo la mkurugenzi linawataka wakope pikipiki kwa
lazima, ambapo kila mwezi kutakatwa shilingi elfu hamsini.
Watumishi
hao wamedai kuwa pamoja na kukopeshwa kwa nguvu pikipiki hizo hakuna hata mmoja
aliyekabidhiwa nakala ya mkataba wa ukopaji huo ambapo nakala zote zimebaki
mkononi mwa mkurugenzi hali ambayo wanaitilia shaka huenda zimetolewa na
serikali kwa ajili ya kusambazwa kwa watumishi wake bure.
Hata hivyo mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya
ya Shinyanga, Mohamed Kiyungi alipotafutwa na waandishi wa habari alikiri
watumishi kutakiwa kukopa pikipiki hizo na kwamba lengo ni kutaka kuhakikisha
wanawajibika kikamilifu katika utendaji kazi wao wa kila siku.
Aidha amesema
ofisi yake imetoa maelekezo pikipiki hizo zitumike kwa shughuli za kiofisi tu
badala ya shughuli binafsi kwa vile kila mwezi watendaji hao wa kata watakuwa
wakilipwa fedha za kununulia mafuta lita 10 na kwamba siyo rahisi kwa mafuta
hayo kutumika katika vyombo binafsi.
| | | | |
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527
Post a Comment