MTOTO MCHANGA AKUTWA AMEKUFA JALALANI

 
Katika hali isiyo ya kawaida maiti ya mtoto mchanga imekutwa imetupwa katika eneo la kuhifadhia taka "jalala" huko Mbagala Nzasa A, maiti ya kichanga hicho ilikutwa ikiwa inatoa harufu huku mwili wake ukiwa umeharibika vibaya kutokana na kuliwa na wadudu.
Walioshuhudia tukio hilo wamesema  maiti ya kichanga hicho ilikuwa  imefungwa katika kanga yenye rangi nyeupe na bluu huku idadi kubwa ya Nzi ikiwa inazonga maiti hiyo  ikiwa imeharibika vibaya sana.
 Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo akiongea kwa masikitiko makubwa alidai kuwa siyo mara ya kwanza tukio hilo kutokea katika eneo hilo kwani miaka miwili nyuma tukio kama hili liliwahi kutokea na mhusika alikamatwa baada ya uchunguzi wa kina uliofanywa na polisi wakisaidiana na raia wema.
Naye mjumbe wa eneo hilo Bwana Saidi Kitambulio alishangazwa na kutokea kwa tukio hilo la kustaajabisha na kulaani vikali na kusema kuwa wametoa taarifa  kituo cha polisi cha jirani ambapo jeshi la polisi litaendelea na utaratibu wake wa kawaida wa kumtafuta muhalifu aliyemtupa mtoto huyo eneo hilo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post