MFANYABIASHARA APIGWA RISASI NA MAJAMBAZI JIJINI MBEYA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi  
Taarifa zilitufikia, zinasema kuwa, mfanyabiashara wa simu eneo la Ilomba Jijini Mbeya, amepigwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi usiku wa kuamkia leo, alipokuwa akielekea nyumbani kwake.
Imeelezwa kuwa alitoka dukani kwake ambako anauza simu akielekea nyumbani kwake eneo la Isyesye Nanenane, ndipo alipovamiwa na watu hao kisha kumpiga risasi ya mguuni na kumpora fedha na gari lake na sasa amelezwa hospitali ya rufaa ya Mbeya kwa ajili ya matibabu.
Jeshi la polisi mkoani Mbeya, linaendelea kuwasaka watu hao. 
 credit-kalulunga blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post