CHADEMA WAIBOMOA KAMBI YA ZITTO KAHAMA,WAMKATAA DIWANI WAO,DIWANI ASEMA ZITTO NI RAFIKI YAKE NDANI NA NJE YA CHAMA

Katibu wa siasa na uenezi wa CHADEMA taifa John Mnyika akizungumza mjini Shinyanga baada ya kutoka Kahama ambapo Chopa yao waliyokuwa wanaitumia kupotea katika eneo la Ubagwe
 hivyo hawakufanikiwa kufika katika eneo hilo walikopaswa kufanya mkutano  ambapo uchaguzi mdogo wa kiti cha udiwani unatarajiwa kufanyika kutokana helikopta waliyokuwa wakitumia kupotea njia na kutua sehemu nyingine na hivyo kufanya safari yao kuihairisha na kuelekea mjini Shinyanga kwa ajili ya mkutano na wananchi.



Chama cha Demokrasia na Maendeleo nchini kimemkataa diwani wake wa Kata ya Majengo wilayani Kahama mkoani Shinyanga Bobson Wambura kwa madai kuwa ni msaliti na anahujumu chama hicho.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara mjini Kahama mkoani Shinyanga katibu wa siasa na uenezi wa Chadema taifa John Mnyika katika moja ya mikutano ya chama hicho ijulikanayo kama Operesheni Pamoja Daima alisema hawatakubali katika chama chao kuwa na watendaji wasaliti.

Alisema hivi sasa wapo katika kazi ya kuwaondoa watu kama Diwani huyo wa kata ya Majengo ambaye walimwita ni msaliti mkubwa wa chama hicho na alipaswa kuondolewa kabisa kwenye chama hicho.

Mnyika alisema moja ya sababu zilizofanya diwani huyo kuondolewa katika chama hicho ni madai ya kwamba alishiriki katika kufanikisha chama hicho kisipeleke mgombea udiwani katika kata ya Ubagwe wilayani Kahama  katika uchaguzi wa mdogo wa udiwani unaotarajiwa kufanyika kutokana na aliyekuwa diwani wa kata hiyo Robert Mndula kufariki dunia mwaka jana.

Aliitaja sababu nyingine kuwa ni madai ya kuwa diwani huyo alikuwa akizunguka mitaani na kuwaambia watu kuwa baadhi ya viongozi wa CHADEMA walitoa kiasi cha shilingi milioni tano ili kuwashinikiza wananchi wahudhurie katika mkutano JANA wa chama hicho mjini Kahama.

“Mimi ndiye katibu mwenezi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo hapa nchini na Bobson ni Katibu  Mwenezi wa Wilaya ya Kahama je, Wananchi mnaniruhusu nimwondoe diwani huyo”, alihoji Mnyika.

Akizungumza na waandishi wa habari kwa njia ya simu akiwa jijini Mwanza Diwani wa Kata ya Majengo Bobson Wambura alisema tuhuma hizo siyo za kweli na kwamba viongozi wa Chadema wameamua kufanya hivyo kwa ajili msimamo wake na aliyekuwa naibu katibu mkuu wa chama hicho Zitto Kabwe.

“Zitto Kabwe ni rafiki yangu iwe ndani ya chama au nje ya chama na nipo tayari kwa lolote watakaloamua wenyewe mimi Chadema siyo yangu kwani hapo zamani nilikuwa naishi kwa udiwani au chama?”, alisema Wambura.

 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments