Taarifa zilizoufikia mtandao huu wa malunde1.blogspot.com asubuhi hii zinasema kuwa malori zaidi ya 40 yamezuia
njia kufuatia tukio la kutekwa kwa madereva wenzao watatu wa malori na
majambazi kisha kucharangwa mapanga,na inasemekana baada ya tukio hilo
kutokea polisi walichelewa kufika eneo la tukio.
Mbali
na malori kuna Mabasi ya abiria na magari binafsi ambayo nayo hayawezi
kupita kufuatia agizo la madereva hao ambao wamesema hawaachii njia
mpaka Mkuu wa Mkoa wa Tabora au kamanda wa polisi mkoa wa Tabora afike,huku wakidai kuwa eneo hilo limekua ni
tatizo sugu kutokana na kutokea vitendo vya utekaji mara kwa
mara.
Eneo
hili linaitwa Iduguta mpakani mwa eneo la Ziba ambalo lipo takribani kilomita 20 kutoka Nzega Mjini,madereva hao wa malori wameziba njia
tangu saa 3 asubuhi hii,japo taarifa inasema tukio la kutekwa kwa
madereva hao limetokea jana saa 3 usiku.
Social Plugin