Mauaji ya kutisha waendesha bodaboda!!! WAENDESHA BODABODA WAWILI WAUAWA NA WATU WALIOJIFANYA WATEJA


Hofu imetanda kwa waendesha pikipiki maarufu bodaboda  na jamii kwa ujumla kufuatia mauaji ya kutisha ya waendesha pikipiki ambao wameuawa kikatili kwa kuchomwa na vitu vyenye ncha kali katika vichwa vyao na watu wanaodaiwa kuwa wateja wao.

Tukio la kwanza  limetokea katika eneo la Bushushu kata ya Ngokolo katika manispaa ya Shinyanga saa mbili asubuhi ambapo  Iddy Omari (27) mwendesha pikipiki mkazi wa mtaa wa Lumumba mjini Shinyanga aligundulika kuuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali kichwani upande wa kushoto na mbinu iliyotumika ni mtu huyo asiyefahamika aliyejifanya mteja na kumkodi mwendesha bodaboda  Desemba 29 mwaka 2013 kwenda eneo la Bushushu alikokutwa ameuawa.

tukio la pili limetokea Desemba 30 mwaka 2013 katika eneo la Mbugani kijiji cha Gembe kata ya Kagongwa wilayani Kahama mkoani Shinyanga ambapo majira ya saa moja asubuhi mwendesha pikipiki aitwaye Gwambo Laurent (27) aligundulika akiwa ameuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali mara tatu kichwani na watu wanaodaiwa kuwa ni wanyang’anyi.


Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Evarist Mangala amesema katika matukio yote mawili waendesha pikipiki hao wawili  yametokea Desemba 30 mwaka 2013 na walinyang’anywa pikipiki zao na amewataka waendesha pikipiki kuchukua tahadhari za kiusalama pindi wanapokuwa kazini nyakati za usiku.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments