Kishapu Yazinduka !!! FUATILIA HAPA HABARI NA PICHA JUU YA UJENZI WA KITUO KIPYA CHA MABASI WILAYANI HUMO

Awali afisa biashara wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu(aliyesimama) bwana Mwafongo Konisaga akimkaribisha afisa habari,mawasiliano na uhusiano wa wilaya ya Kishapu  mkoani Shinyanga John Mlyambate katika ukumbi wa mikutano wa wilaya hiyo wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari kuzungumzia hali halisi ya maendeleo katika wilaya hiyo ambapo kituo  kipya cha mabasi  kitajengwa katika eneo la kijiji cha Isoso kata ya Kishapu wilayani humo.

Afisa habari,mawasiliano na uhusiano wa wilaya ya Kishapu  mkoani Shinyanga John Mlyambate akizungumza na waandishi wa habari leo ambapo amesema halmashauri ya wilaya ya Kishapu imeanza rasmi ujenzi wa kituo hicho kwa kiwango cha changarawe  mwezi Oktoba mwaka huu na utakamilika mwezi Juni mwaka 2014 na hadi kukamilika kwake utagharimu shilingi bilioni moja

Ni katika eneo la kijiji cha Isoso kata ya Kishapu kunakojengwa stendi ya mabasi yatokayo na kuingia katika wilaya ya Kishapu.Uchimbaji wa misingi kama unavyoona unaendelea

Misingi inaendelea kuchimbwa.Katika kituo hicho cha mabasi kutakuwa na zaidi ya vibanda 300 kwa ajili ya wafanyabiashara hivyo stendi hiyo itawanufaisha wakazi wa eneo hilo siyo tu kutatua kero ya usafiri lakini pia ajira
 wakazi wa wilaya hiyo kwa muda mrefu wamekosa eneo rasmi kwa ajili ya huduma ya usafiri hivyo wakati mwingine wakijikuta wakikosa usafiri kutokana na kukosa eneo maalum kwa ajili ya kusubiri usafiri.Ujenzi wa kituo hicho utakuwa neema kwao
Kwa mujibu wa afisa habari John Mlyambate mradi huo unajengwa kwa kutumia fedha ambazo halmashauri imekopa kutoka bodi ya mikopo ya serikali za mitaa kiasi cha shilingi 800,000,000/= ambapo halmashauri tayari imechangia shilingi 200,000,000/= ili kukamilisha thamani ya mradi huo ambapo ni shilingi bilioni moja
Tayari wakazi wa eneo hilo wameanza kunufaika na ujenzi huo.Hapo juu ni bi Kadogo Tophil ,mwanamke pekee ambapo kamera za  Malunde Blog zilifanikiwa  kumnasa akichimba msingi,ambapo kwa mujibu wa maelezo yake ukichimba umbali wa mita moja ,ikiwa urefu kwenda chini ni mita 2 na nusu unapatiwa shilingi elfu moja na yeye kwa siku ana uwezo wa kuchimba mita saba

Changarawe tayari zishaanza kusogezwa eneo la mradi wa ujenzi wa stendi ya mabasi katika wilaya hiyo
Hapa ni katika moja ya eneo la mji wa Mhunze wilayani Kishapu kama unavyoona hapo juu magari madogo yamepaki kutokana na kukosa eneo maalum kwa ajili ya kupaki.Hapo ni karibu na barabara ambako wakazi wa eneo hilo hulazimika kuvizia magari kwa ajili ya usafiri

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post