Hali ni tete!!! KIKONGWE AUA MTU HUKO KAHAMA CHANZO CHADAIWA KUWA NI MGOGORO WA MASHAMBA

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Evarist Mangala
Mzee Charles Abdallah Makune(87) mkazi wa kijiji cha Kahanga kta ya Wendele wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga amemuua kwa kumpiga risasi kichwani Mihangwa Maziku maarufu kwa jina la Mambe(40) mkazi wa kijiji hicho kutokana na kile kilichodaiwa  kuwa ni mgogoro wa  mashamba.

Kamanda wa jeshi  la polisi mkoani hapa Evarist Mangala tukio hilo amesema tukio hilo limetokea juzi  majira ya saa moja asubuhi ambapo Mihangwa Maziku akiwa nyumbani kwake alipigwa risasi kichwani na  mzee Charles Abdallah Makune .

Amesema tukio hilo lilitokea  baada ya kutokea hali ya kutoelewana kati yao katika mgogoro wa mashamba.

Kufuatia tukio hilo wananchi walimshambulia kikongwe huyo kwa kumpiga na kitu kizito kichwani hali iliyosababisha kikongwe huyo apelekwe katika hospitali ya wilaya ya Kahama kupatiwa matibabu ingawa hata hivyo kikongwe huyo alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post