Madaktari nchini Kenya wameelezea wasiwasi kuhusu matumizi mabaya na
ya kiholea ya dawa za dharura ambazo zinanuiwa kuwakinga waathiriwa wa
ubakaji kutokana na maambukizi ya virusi vya HIV.
Dawa hizo
zinazojulikana kama PEPS, zinapaswa kupewa mwathiriwa baada ya daktari
kuthibitisha kuwa kweli yuko katika hali ya hatari ya kuambukizwa virusi
vya HIV, na hutolewa tu na wataalamu wa matibabu ya HIV.
Lakini mwandishi wa BBC Zainab Deen aligundua kuwa wanawake makahaba wamegundua njia za kupata dawa hizo.
BBC
Post a Comment