MAJAMBAZI YATEKA BASI KATIKA DARAJA LA 54 SHINYANGA




Watu wasiojulikana wanaodhaniwa kwa ni majambazi wakiwa na mawe na mapanga wameteka magari mawili likiwemo basi la Nkamba’s  kisha kupora fedha na simu za abiria na kujeruhi sita usiku wa kuamkia leo katika barabara ya Shinyanga -Mwanza.

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Evarist Mangalla amesema tukio hilo limetokea  leo saa sita usiku katika daraja  la 54 katika kijiji cha  Buchambi kata ya Mwadui-Luhumbo wilayani Kishapu.

 Magari yaliyotekwa kuwa  ni pamoja na Basi la kampuni ya Nkamba’s lenye namba za usajili T610 ARR scania pamoja na gari lenye namba za usajili T722 CKZ aina ya Fuso  ,yote yakitokea jijini Dar es salaam kuelekea jijini Mwanza.

katika tukio hilo abiria wameporwa simu na fedha ambazo hazijajulikana idadi wala thamani yake.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post