MTOTO ABAKWA, AUAWA KISHA KUWEKWA KWENYE BOKSI

Mwili wa mtoto aliyebakwa na kuuawa kisha kuwekwa kwenye boksi

Mtoto mmoja anayekadiriwa kuwa na miaka kati ya kumi na mbili hadi kumi na tatu,mwenye jinsia ya kike,asiyefahamika jina wala makazi yake amekutwa akiwa ameuawa katika eneo Ngokolo mitumbani karibu na jalala la takataka mjini shinyanga.

Kamanda wa polisi mkoa wa shinyanga ACP Evarist Mangalla amethibitisha kutokea kwa tukio hilo jana maiira ya saa tano asubuhi na kuongeza kuwa mtoto huyo mwenye jinsia ya kike alikutwa akiwa ameuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani na kisogoni kisha mwili wake kuwekwa kwenye boksi na kufungwa kwa kamba za katani.

Kamanda MangallA amesema uchunguzi wa daktari unaonesha kuwa mtoto huyo alibakwa kabla ya kuuawa na kuongeza kuwa jeshi la polisi bado linaendelea kufanya uchunguzi ili kuwabaini na kuwakamata watu waliohusika katika mauaji hayo kwani mpaka  sasa chanzo cha mauaji hakijulikani.

Kamanda wa polisi mkoani hapa anatoa wito kwa wananchi kutoa taarifa za siri kwa jeshi hilo ili kuweza kuwabaini na kuwakamata watuhumiwa wa tukio hilo.




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments