Na Marco Maduhu
Mtoto mmoja wa kike mwenye umri wa miaka 7 jina lake linahifadhiwa ambaye ni mkazi wa
Kizumbi katika Manispaa ya Shinyanga amefanyiwa ukatili wa ,kijinsia kwa
kuingiliwa kinyume na maumbile na kisha kutobolewa jicho la kulia na kitu
chenye ncha kali na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia Machi 26 mwaka huu.
Mganga wa zamu
katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga Dr, Giliadi Kasoga alikiri kumpokea mtoto
huyo majira ya saa nane usiku kwa ajili
ya matibabu.
"Nime
mpokea mtoto huyo majira ya saa nane usiku, huku akiwa hoi na baada ya kuanza
kumfanyia vipimo na ndipo nilipobaini kuwa alifanyiwa kitendo hicho kinyume na
maumbile ambapo nilikuta michubuko na baadhi ya manii"alisema Dr kasonga
Dr.Kasoga aliendelea kusema kuwa mtoto huyo
alifikishwa hospitalini hapo na jeshi
la sungusungu ambao walisema kuwa
walimkuta mtoto huyo akiwa ametelekezwa katika eneo moja hatarishi huko Kizumbi
mara baada ya kufanyiwa ukatili huo wakati wakiwa katika doria ya usiku.
Kufuatia hali ya
mtoto huyo kutokuwa ya kuridhisha na ndipo walipo amua kumpatia Rufaa ya kwenda
kutibiwa katika hospitali ya Rufaa Bugando
jijini Mwanza kwa matibabu zaidi kutokana na upungufu wa vifaa vya
kitaalamu katika hospitali hiyo ya mkoa wa shinyanga
Kwa upande wao
baadhi ya maafisa wa jeshi la polisi wanaochunguza chanzo cha tukio hilo
walisema kuwa taarifa kamili zitatolewa kupitia kwa kamanda wa jeshi la polisi
wa mkoa wa shinyanga ACP Evarist Mangala mara baada ya uchunguzi wa tukio hilo
utakapo kamilika.