Asilimia 90 ya Vitu Vya Marehemu Sharo Millionea vilivyoibiwa Vyapatikana


Mkuu wa Wilaya ya Muheza pamoja na Jeshi la Polisi la mkoani Tanga limetangaza kuwa baadhi ya vitu vya marehemu Sharo Millionea ambavyo alivyokuwanavyo  wakati wa ajali vimepatikana.
 Vitu hivyo ni pamoja na Simu.Battery ya Gari,Viatu,T-shirt,Jeans,Pete,Cheni na Tairi moja ya gari. 
 Vitu hivyo vimerudishwa na polisi jamii ambao ni wazazi wa wezi hao.
 Aidha pamoja na vitu hivyo kupatikana Jeshi la Polisi bado linaendelea kufanya msako wa kuwapa hao vijana ambao ndo wanasadikika kuwa ndo wezi wenyewe.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments