Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

Tanzia : BWEGE AFARIKI DUNIA



Chama cha ACT Wazalendo kimetangaza kwa masikitiko kifo cha mwanachama wake, Ndugu Seleman Bungara maarufu kama Bwege, kilichotokea ghafla wakati akiwa hospitalini akipatiwa matibabu ya kusafisha figo (dialysis).

Kupitia taarifa iliyotolewa na kiongozi wa chama, Dorothy Semu, chama kimetoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na wanachama wote walioguswa na msiba huo.

ACT Wazalendo imemtaja marehemu Bungara kama mwanasiasa wa upinzani aliyekuwa mstari wa mbele katika kupigania haki na demokrasia nchini.

 Chama hicho kimesema kitashiriki kikamilifu katika mazishi na kuwataka wanachama kuungana na familia katika kipindi hiki kigumu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com