Nilipoajiriwa kazini, nilikuwa na ndoto kubwa. Nilifanya kazi kwa bidii, nilikuwa mtu wa kwanza kufika na wa mwisho kutoka. Kila jukumu nililopewa nililitekeleza kwa uaminifu na kujituma.Nilitarajia juhudi zangu zingeonekana, lakini mwaka wa kwanza ulipita bila mabadiliko yoyote. Nilijipa moyo nikijua labda muda wangu ulikuwa bado haujafika.
Mwaka wa pili ukaanza, na hali ikawa ile ile. Watu niliowafundisha wakaanza kupandishwa vyeo. Wengine waliokuwa na muda mfupi kazini wakawa wakubwa wangu. Nilikuwa nashangaa, nilikuwa naumia kimya kimya.
Social Plugin