Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

DOTTO EMANUEL MANUMBU ASHINDA TUZO YA TOP 100 AFRICANS GLOBAL 2026 KAMA GLOBAL YOUNG MALE POLITICAL LEADER


Kiongozi kijana katika masuala ya Elimu, Habari na Siasa, Dotto Emanuel Manumbu, ametangazwa rasmi kuwa mmoja wa washindi wa tuzo za Top 100 Africans Global 2026, akitambuliwa katika kipengele cha Global Young Male Political Leader.

Tuzo hiyo imetolewa kwa kutambua mchango wake mkubwa katika uongozi na juhudi zake za kuleta maendeleo chanya kwa jamii pamoja na Taifa kwa ujumla. 

Kupitia nafasi mbalimbali za kiuongozi, Manumbu ameonyesha uwezo, ubunifu na dhamira ya dhati katika kutumikia nafasi yake na jamii kwa ujumla. 

Akizungumzia ushindi huo, Manumbu ameeleza kuwa ni heshima kubwa kwake na kwa Tanzania kwa ujumla, akisisitiza kuwa tuzo hiyo ni motisha ya kuendelea kufanya kazi kwa bidii, unyenyekevu, na uadilifu kwa manufaa ya jamii.

“Tuzo hii ya heshima namrejeshea Mungu, ambaye ndiye mgawaji wa riziki na neema zote. Nawashukuru kwa dhati wazazi wangu kwa malezi yao mema, viongozi wangu walionilea na kuniongoza katika utumishi wangu, Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ukerewe kwa kuniamini na kunipa fursa ya kuwatumikia wananchi. Aidha, namshukuru DC Ngubiagai, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri (DED), pamoja na Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT) Tawi la Mwanza — kisima cha kuzalisha viongozi makini barani Afrika. Shukrani za pekee pia ziende kwa watumishi wenzangu wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kwa ushirikiano na malezi yaliyonifikisha katika hatua hii,” amesema Manumbu.

Hafla rasmi ya ugawaji wa tuzo hizo inatarajiwa kufanyika tarehe 28 Februari 2026 katika ukumbi wa Morena Hotel jijini Dodoma, ambapo washindi kutoka mataifa mbalimbali barani Afrika watatunukiwa tuzo hizo rasmi.

Ushindi huo umeendelea kuiweka Tanzania katika ramani ya kimataifa kwa kuonyesha mchango wa vijana katika uongozi na maendeleo ya Bara la Afrika.




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com