Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MAKAMU WA RAIS MHE. DKT. EMMANUEL NCHIMBI AMTEMBELEA MAKAMU WA RAIS MSTAAFU DKT. MOHAMED GHARIB BILAL



Na Mwandishi wetu, Dar

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, leo tarehe 02 Januari 2026 amemtembelea na kumjulia hali Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal, katika makazi yake yaliyopo Masaki jijini Dar es Salaam.

Katika ziara hiyo ya heshima na utu, Dkt. Nchimbi ameeleza dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuendelea kuthamini mchango wa viongozi wastaafu katika ujenzi wa Taifa, akisisitiza kuwa uzoefu na busara zao ni hazina muhimu kwa maendeleo ya nchi.

Kwa upande wake,  Dkt. Gharib Bilal amemshukuru Makamu wa Rais kwa kumtembelea, akieleza kufarijika na kuendelea kwa mshikamano na mawasiliano kati ya viongozi walioko madarakani na wale waliotumikia Taifa katika vipindi tofauti.

Ziara hiyo imeendelea kudhihirisha utamaduni wa kuheshimiana, kuthaminiana na kudumisha umoja wa kitaifa, sambamba na kuimarisha misingi ya maadili na uongozi bora nchini.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com