Makubel amechukua fomu kwa katibu wa CCM wilaya ya Tanga Jamal Khimji mapema leo asubuhi katika ofisi za chama hicho jiji la Tanga.
Akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kuchukuwa fomu hiyo Makubel amesema kuwa uongozi wa Rais Samia umemvutia kuweza kuona ipo haja kugombea ili kuunga mkono juhudi hizo .
"Nia yangu ni kuomba ridhaa kwa wanaccm kuweza kuwatumika wanatanga hivyo nawaomba waniunge mkono katika dhamira hii ya kuwaletea maendeleo wananchi wenzangu "amesema Amar.
"Nimejitokeza leo kuchukua fomu ili kuwania kuteuliwa na kupata ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi katika jimbo letu la Tanga ili kuweza kupeperusha bendera ya chama chetu katika uchaguzi huu mwezi Oktoba, "amesema Makubel.
Social Plugin