MWENGE - ITV WABORESHEWA MIFUMO YA MAJITAKA

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) imeanza kazi ya kubadili bomba chakavu la Majitaka la inchi 16 na kuweka bomba jipya la ukubwa wa inchi 16 kwa umbali wa mita 90 likiendelea eneo la Mwenge ITV kwa lengo la kuboresha mifumo ya Majitaka iliyo na wateja zaidi ya 1,000.


Kazi hii inalenga kuboresha huduma ya usafi wa mazingira katika maeneo ya Mlimani city, Mwenge kwa masista, Mwenge round about, Mwenge TRA, Zahanati ya Mwenge pamoja na baadhi ya maeneo ya Sinza.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post