VIONGOZI WIZARA YA ELIMU WAKITETA JAMBO NA BABU TALE DODOMA

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Carolyne Nombo wakijadiliana jambo na Mjumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo na Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki Mhe. Shaban Hamis Taletale katika viwanja vya Bunge leo Mei 08, 2024.

Prof. Mkenda aliwasilisha Bajeti ya Wizara hiyo Bungeni, Jana Mei 07, 2024 akiliomba Bunge kuidhinisha zaidi ya Shilingi Trilioni 1.9 zitakazoelekezwa kwenye vipaumbele vitano vinavyolenga kuleta mageuzi ya Elimu nchini huku msukumo mkubwa ukiwekwa kwenye Elimu ya ujuzi ili kuwawezesha wahitimu katika ngazi mbalimbali kujiajiri na kuajiri wengine.

#TunaboreshaElimuYetu 
#ElimuUjuziNdioMwelekeoWetu

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post