NTOBI ANG'ARA... ATOBOA TENA UENYEKITI CHADEMA SHINYANGA

 

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Shinyanga , Emmanuel Ntobi, ameshinda kuwa Mwenyekiti wa Chama hicho mkoani humo, katika uchaguzi wa Machi 28, 2024. 

Katika uchaguzi huo Ntobi alikuwa akichuana na Peter Machaga ambaye alipata kura 26, Ntobi 26 na Thadei Mwati Kura 8. Na ikalazimu kurudiwa kwa duru ya pili ambapo Ntobi alichuana na Machaga na kuibuka na kura 33 sawa na asilimia 55, na Machaga kuibuka na kura 27.

Hivyo Msimamizi mkuu wa uchaguzi Suzani Kiwanga (ambaye ni mjumbe wa kamati kuu CHADEMA) alimtangaza Ntobi kuwa Mwenyekiti wa Mkoa wa Shinyanga.


Ntobi anakuwa ni Mwenyekiti wa Chama hicho kwa kipindi cha pili 2024 hadi 2029.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments