TAASISI YA NELSON MANDELA YAHAMASISHA WASICHANA KUPENDA SAYANSI

 

Naibu Makamu Mkuu wa Taasisi Mipango, Fedha na Utawala wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Neslon Mandela Prof. Suzana Augustino akichangia katika mdahalo wakati wa maadhimisho ya Kimataifa ya siku ya Wanawake na Wasichana katika Sayansi Jijini Arusha.

Na Mwandishi Wetu.

Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela inashiriki kikamilifu katika kuleta hamasa na chachu ya Wasichana na Wanawake kupenda na kujiunga na masomo ya Sayansi, Hisabati, Teknolojia, Uhandisi na Ubunifu katika kuongeza wataalam wa fani hizo nchini.

Hayo yamesemwa Jijini Arusha na Naibu Makamu Mkuu wa Taasisi Mipango,Fedha na Utawala wa Taasisi hiyo, Prof. Suzana Augustino wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Siku ya Wanawake na Watoto katika Sayansi iliyofanyika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC jjini hapo.

"Katika kulitekeleza hili mbali na kutoa mafunzo ya Shahada ya Uzamili na Uzamivu pia tunatoa hamasa kwa wanafunzi wa elimu ya Msingi na Sekondari ili wapenda masomo ya sayansi, Hisabati, Teknolojia, Uhandisi na Ubunifu kupitia klabu na vikundi vinavyofanya kazi na watafiti wetu" amesisitiza Prof. Suzana Augustino.

Ameongeza kuwa, taasisi imekuwa ikifanya kazi kwa kushirikiana na shule za msingi na sekondari kwa kutoa utaalamu kupitia wabunifu wake katika kuwafundisha wanafunzi kwa vitendo kupitia nyanja mbalimbali.

“Kuna shule ambayo watoto wanajifunza mambo ya nishati mbadala ambapo taasisi yetu inatoa utaalamu lakini wao wanafanya kwa vitendo, kwa kufanya hivyo miaka mitano ijayo tutakuwa na watoto wanaopenda masomo ya sayansi na hivyo kuchangia katika adhma ya serikali ya kuongeza idadi na ushiriki wa wanawake na wasichana katika sayansi” ameeleza Prof. Suzana Augustino.

Naye Mhadhiri kutoka Taasisi hiyo Prof. Neema Kassim ametoa wito kwa jamii kuwapa nafasi watoto ya kushiriki masomo ya vitendo ili kuweza kupenda wanachofanya kwa kuwashirikisha katika midahalo mbalimbali ili kuwa na uwezo wa kujiamini.

Maadhimisho ya siku ya wanawake na wasichana katika sayansi mwaka huu yameongonzwa na Kauli Mbiu “Wanawake na wasichana katika Uongozi wa Sayansi, Enzi Mpya ya Maendeleo Endelevu”.

Waziri wa Elimu ,Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda akiongea katika maadhimisho ya Kimataifa ya siku ya Wanawake na Wasichana katika Sayansi tarehe 11 Februari,2024 Jijini Arusha.

Naibu Makamu Mkuu wa Taasisi Mipango, Fedha na Utawala wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Neslon Mandela Prof. Suzana Augustino akichangia katika mdahalo wakati wa maadhimisho ya Kimataifa ya siku ya Wanawake na Wasichana katika Sayansi Jijini Arusha.

Mhadhiri kutoka Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof. Neema Kassim akichangia katika mdahalo katika maadhimisho ya Kimataifa ya siku ya Wanawake na Wasichana katika Sayansi Jijini Arusha.

Mhadhiri Mstaafu Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof. Verdiana Masanja akisoma risala wakati maadhimisho ya Kimataifa ya siku ya Wanawake na Wasichana katika Sayansi Jijini Arusha.

Wanafunzi kutoka shule za Sekondari na Msingi jijini Arusha wakifuatilia matukio mbalimbali katika maadhimisho ya Kimataifa ya siku ya Wanawake na Wasichana katika Sayansi Jijini Arusha.

Waziri wa Elimu ,Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Taasisi za Elimu za juu wakati wa maadhimisho ya Kimataifa ya siku ya Wanawake na Wasichana katika Sayansi Jijini Arusha.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post