WAWEKEZAJI WAMIMINIKA KIJIJI CHA NGURUWE DODOMA: BEN POL AWEKEZA MILIONI 8, DOTTO MAGARI MILIONI 70



Historia imeandikwa Dodoma!! Mwenyeji wa Mkoa wa Dodoma Msanii Ben pol ameamua kumuunga mkono msanii mwenzake Prof. Jay na Mke wake Prof. Jay katika uwekezaji wa ufugaji wa nguruwe katika kijiji cha Nguruwe Dodoma.

Msanii Ben Pol ametembelea Mradi wa Kijiji cha Nguruwe Novemba 2,2023 ambapo amewekeza kiasi cha shilingi milioni 8 huku akiwahamasisha Watanzania na Watanzania waishio nje ya nchi na wageni kuja kuwekeza katika mradi huo wa Nguruwe.

Sambamba na Uwekezaji huo Msanii Ben Pol amepokea Hundi ya Milioni 16 kutoka kwa Mkurugenzi Bi. Grace Mgonjo ambaye ni Mke wa Msanii Maarufu nchini na Mwanasiasa Joseph Haule ‘Prof. Jay’.

Ben Pol amempongeza Mke wa Prof. Jay kwa kuibua fursa hiyo adimu na kuahidi kuwaalika wasanii wenzake pamoja na wafuasi wake zaidi ya milioni 4 na laki 8 kuwekeza katika mradi huo.

Naye Dotto Ketto (Dotto Magari) amewekeza Shilingi milioni 70 sambamba na kukabidhiwa hundi ya milioni 140 na Grace Mgonjo ( mke wa prof Jay ambapo anatarajia kwenda bank na bila kupitia ofisi za Piginvest International Plc kwa vile check iko tayari baada ya miezi 6.
Mke wa Prof. Jay amewaasa Watanzania na Watu wote Duniani waje kuwekeza pesa zao ili wapate faida mara mbili ya mtaji wao baada ya miezi 6.

Mwenyekiti Wa Zamahero bwana Wiliam amewakaribisha watanzania kuja kumuunga mkono mke wa Prof. Jay na kumshukuru kwa fursa za ajira hasa wanawake wa Zamahero ambao sasa hawahangaiki tena na hali mbaya ya uchumi ambayo imekuwa ikiwakumba.

Nao Wananchi wa Zamahero Dodoma wameipongeza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira mazuri ya wawekezaji na hivyo kuvuta wawekezaji wengi na kuchochea ajira hususani kwa wanawake.

Mradi huu wa nguruwe unaenda kuweka zaidi ya shilingi Bilioni 270 ambapo njia ambayo inatumika ni njia ya Clusters au njia ya mabanda shufwa(block farming).

Kwa ajili ya kumuunga mkono Mke wa Prof. Jay Mpigie kwa 0627122122 au 0627188188 bure





















Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post