PACESH YATOA ELIMU YA SHERIA YA NDOA, KUPINGA UKATILI KIJINSIA KWA WANANCHI WA WISHITELEJA KISHAPU

Meneja Miradi kutoka Shirika la Msaada wa Kisheria mkoani Shinyanga PACESH John Shija, akitoa elimu sheria ya ndoa, na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wananchi wa Wishiteleja wilayani Kishapu.

Na Marco Maduhu, KISHAPU

SHIRIKA linalotoa msaada wa kisheria mkoani Shinyanga Paralegal Aid Centre (PACESH), limetoa elimu ya Sheria ya ndoa, kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wananchi wa Kijiji cha Wishiteleja wilayani Kishapu ikiwamo jamii kuacha kuozesha watoto ndoa za utotoni,pamoja na wanandoa kuacha kuishi kienyeji bila kuwa na vyeti vya ndoa.

Elimu hiyo imetolewa leo Oktoba 25, 2023 katika Kijiji cha Wishiteleja Kata ya Mondo wilayani Shinyanga, mafunzo ambayo yamewezeshwa na Shirika la WiLDAF kupitia Shirika la Idadi ya Watu la Umoja wa Mataifa UNFPA.
Meneja Miradi Shirika la PACESH John Shija, akizungumza katika utoaji wa elimu hiyo, amewataka wananchi wa Kijiji hicho cha Wishiteleja, kuachana na tabia ya vitendo vya ukatili wa kijinsia ikiwamo kuozesha watoto ndoa za utotoni, vipigo kwa akina mama, pamoja na kuacha kunyimana tendo la ndoa ili kuimarisha ustawi wa familia na kuishi kwa upendo na amani.

Aidha, amewataka pia wanandoa kuacha tabia ya kuishi kienyeji bila ya kuwa na cheti cha ndoa, aidha cha Kimila au Kanisani, bali wanapaswa kuwa nacho kwa sababu kina umihumu wake hasa katika suala la Migogoro ya Mirathi au kugawana Mali pale ndoa inapovunjika.
“Watu wamekuwa wakiishi kienyeji kama Mke na Mume bila ya kuwa na cheti cha Ndoa, siku likitokea tatizo ndiyo mtajua umuhimu wake, acheni kuishi kienyeji kuweni na vyeti vya ndoa aidha cha Kimila au Kanisani vitawasaidia sababu ndoa yako itakuwa halali ina udhibitisho,”amesema Shija.

Katika hatua nyingine amewataka wazazi kutekeleza majukumu kwa watoto wao, ikiwamo kuwasomesha na kuwatimizia mahitaji yote ya shule, na kwa watoto wale ambao wameshindwa kuendelea na msomo kwa sababu mbalimbali watumie fursa ya kusomeshwa bure na WiLDAF katika Chuo cha VETA Kishapu, na kupata ujuzi ambao utawaendeleza katika maisha yao.
Nao Wananchi waliopata elimu hiyo wamelishukuru Shirika hilo la PACESH kwa kuwapatia elimu hiyo ambayo itawasaidia katika maisha yao kwa kuacha vitendo vya ukatili, pamoja na kutafuta vyeti vya ndoa vya kimila na kuacha kuishi kienyeji.
Meneja Miradi kutoka Shirika la Msaada wa Kisheria mkoani Shinyanga PACESH John Shija, akiendelea kutoa elimu sheria ya ndoa, na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wananchi wa Wishiteleja wilayani Kishapu.
Meneja Miradi kutoka Shirika la Msaada wa Kisheria mkoani Shinyanga PACESH John Shija, akiendelea kutoa elimu sheria ya ndoa, na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wananchi wa Wishiteleja wilayani Kishapu.
Meneja Miradi kutoka Shirika la Msaada wa Kisheria mkoani Shinyanga PACESH John Shija, akiendelea kutoa elimu sheria ya ndoa, na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wananchi wa Wishiteleja wilayani Kishapu.
Meneja Miradi kutoka Shirika la Msaada wa Kisheria mkoani Shinyanga PACESH John Shija, akiendelea kutoa elimu sheria ya ndoa, na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wananchi wa Wishiteleja wilayani Kishapu.
Meneja Miradi kutoka Shirika la Msaada wa Kisheria mkoani Shinyanga PACESH John Shija, akiendelea kutoa elimu sheria ya ndoa, na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wananchi wa Wishiteleja wilayani Kishapu.
Meneja Miradi kutoka Shirika la Msaada wa Kisheria mkoani Shinyanga PACESH John Shija, akiendelea kutoa elimu sheria ya ndoa, na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wananchi wa Wishiteleja wilayani Kishapu.
Meneja Miradi kutoka Shirika la Msaada wa Kisheria mkoani Shinyanga PACESH John Shija, akiendelea kutoa elimu sheria ya ndoa, na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wananchi wa Wishiteleja wilayani Kishapu.
Meneja Miradi kutoka Shirika la Msaada wa Kisheria mkoani Shinyanga PACESH John Shija, akiendelea kutoa elimu sheria ya ndoa, na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wananchi wa Wishiteleja wilayani Kishapu.
Meneja Miradi kutoka Shirika la Msaada wa Kisheria mkoani Shinyanga PACESH John Shija, akiendelea kutoa elimu sheria ya ndoa, na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wananchi wa Wishiteleja wilayani Kishapu.
Meneja Miradi kutoka Shirika la PACESH John Shija (kushoto) akiteta jambo na Mtendaji wa Kijiji cha Wishiteleja wilayani Kishapu Daudi John.
Mtendaji wa Kata ya Mondo Dotto Mnyama akizungumza kwenye Mkutano huo.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Wishiteleja William Ndodi akizungumza kwenye Mkutano huo.
Wananchi wakisiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Mwananchi akiuliza maswali ya sheria ya ndoa kwenye mkutano huo.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Mwananchi akiuliza maswali kwenye Mkutano huo.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Mkutano ukiendelea wa Elimu ya Sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa Kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya sheria ya ndoa na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post