NEMC YAPOKEA MALALAMIKO ZAIDI YA 230 KUTOKANA NA KELELE ZILIZOZIDI KIWANGO

Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa na Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dk. Samuel Gwamaka akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 12,2023 katika Ofisi za NEMC Jijini Dar es Salaam

******************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

BARAZA la Taifa na Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeendelea kuwaonya wamiliki wa baa na kumbi za starehe kwa kuendelea na uchafuzi wa mazingira kutokana na kelele hivyo watachukuliwa hatua kali ikiwemo kufungiwa biashara zao.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 12,2023 Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dk. Samuel Gwamaka, amesema uchafuzi wa mazingira unaotokana na kelele umeanza upya na tayari wamepokea malalamiko zaidi ya 230.

Amesema kumekuwa na ongezeko kubwa la uchafuzi wa mazingira kwa kelele zilizopita viwango licha ya baraza hilo kutoa elimu kwa umma na wamiliki wa kumbi hizo na baa.

“Tuliokuwa tumewafungia walitii wakatimiza masharti tuliyowapa tukawafungulia lakini ndani ya mezi mitatu tumepata malalamiko zaidi ya 230 ya kelele kwa hiyo tunawaonya waachane na kelele kabla hatujaanza kuchukua hatua kali kama zilizopita,”Amesema

Aidha Dkt.Gwamaka amesema wote waliokuwa wamefungiwa walifunguliwa na kuendelea na biashara zao kama kawaida lakini katika siku za karibuni wamejisahau baada ya kuona utulivu na wameanza tena kupiga kelele hizo tena.

Pamoja na hayo amewakumbusha wamiliki hao kuwa sheria bado ipo na inafanyakazi na NEMC itaendelea kuwaelimisha kwamba kelele ni uchafuzi lakini wale watakaokaidi haitasita kuwachukulia hatua kama za hivi karibuni.

“Si kwamba NEMC inaona sifa kufunga biashara ya mtu, tunajua biashara hizo zimeajiri watu wengi sana na zinalipa kodi lakini kelele nazo zimekuwa zikisababisha athari kubwa kwa wananchi kwa hiyo fanya biashara yako bila kuathiri maisha ya mtu mwingine,” Amesema Dkt.Gwamaka
Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa na Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dk. Samuel Gwamaka akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 12,2023 katika Ofisi za NEMC Jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa na Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dk. Samuel Gwamaka akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 12,2023 katika Ofisi za NEMC Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE EMMANUEL MBATILO)

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post