NYUKI WAZUA TAHARUKI BAADA YA KUVAMIA HARUSI....WAGENI WAAMBULIA NUNDU


Video moja inasambaa mitandaoni ikionyesha tukio ambapo kundi la nyuki kuwavamia wageni kwenye hafla ya harusi katika Jimbo la Anambra, Nigeria.

Wageni hao walikuwa wamekusanyika kusherehekea pamoja na maharusi wakati kundi la nyuki lilipotokea ghafla na kuanza kuwashambulia na kusababisha hali ya mtafaruku.

Katika video ya harusi hiyo inayoendelea kusambaa mtandaoni kama moto, wageni waliohudhuria karamu hiyo wanaonyeshwa wakipiga kelele kwa hofu na kukimbia pande tofauti huku nyuki wakiwavamia kwa wingi. 

Inaripotiwa kwamba nyuki hao walikatiza harusi hiyo kwa sababu ilipangwa katika siku maalum ya soko na tayari walikuwa wameonywa.
 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments