LEMBELI ASHIRIKI SHEREHE YA MWANZILISHI WA TAASISI YA JANE GOODALL NCHINI MAREKANI


Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama-James Lembeli ( maarufu Ng'wana Maria) katika picha kwenye hafla ya kumpongeza Mwanzilishi wa Taasisi ya Jane Goodall Dk. Jane Goodall na Balozi wa heshima wa Umoja wa Mataifa wa Amani kutimiza miaka 89 iliyofanyika katika Hotel ya Litz Carlton, New York - Marekani iliyohudhuriwa na wanasayansi,wahifadhi,Wana mazingira na viongozi mbalimbali duniani.


Dk. Jane Goodall alifika Tanzania, wakati huo Tanganyika mwaka 1960 na kuanzia utafiti wa wanyama aina ya Sokwe katika hifadhi ya Gombe utafiti ambao unaendelea mpaka leo.

Katika ghafla hiyo,watu mbalimbali walimtakia Jane Goodall afya njema na maisha marefu.
Pia walimpa zawadi ikiwa pamoja pesa,ambazo zote zitapelekwa Gombe, Kigoma kuendeleza kazi za utafiti na uhifadhi katika Hifadhi hiyo nchini Tanzania.
Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama, James Lembeli akizingumza na Dk. Jane Goodall.
Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama, James Lembeli katika picha ya pamoja na baadhi ya waalikwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments