SIKUKUU YA EID- EL-FITR NI KESHO JUMAMOSI


Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir amesema Sikukuu ya Eid el-Fitr itakuwa Jumamosi ya Aprili 22, 2023.

Sikukuu hiyo Kitaifa itafanyikia jijini Dar es Salaam ambapo Swala ya Eid itaswaliwa Msikiti wa Mfalme Mohamed VI Bakwata Makao Makuu, Kinondoni kuanzia saa 1:30 asubuhi na kufuatiwa na Baraza la Eid litakalofanyika ukumbi wa Mwalimu Nyerere kuanzia saa 8:30 mchana.

Katika Baraza hilo, inatarajiwa kuhudhuriwa na wageni mbalimbali wakiongozwa na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments