CCM YARIDHISHWA NA UTENDAJI WA MADAKTARI HOSPITALI YA RUFAA YA BOMBO


Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani kulia akieleza jambo kwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajabu Abdurhaman wakati wa ziara ya Kamati ya Siasa Mkoa wa Tanga kutembelea Kambi ya Matibabu ya Madaktari Bingwa kutoka Hospitali ya Benjamini Mkapa Dodoma walioweka kambi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo katikati aliyevaa koti la bluu ni Katibu wa Hospitali hiyo Abdiely Makange
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajabu Abdurhaman akisikiliza maelezo kwa Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani ambaye hayupo pichani wakati wa ziara ya Kamati ya Siasa Mkoa wa Tanga kutembelea Kambi ya Matibabu ya Madaktari Bingwa kutoka Hospitali ya Benjamini Mkapa Dodoma walioweka kambi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo kushoto ni Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Suleiman Mzee na kulia aliyesimama ni Katibu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Abdiely Makange
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajabu Abdurhaman akimsikiliza kwa umakini Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani kulia aliyevaa koti jeupe na wa pili kushoto aliyevaa koti la bluu ni Katibu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Abdiely Makange
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajabu Abdurhaman akizingumza mara baada ya kutembelea kambi ya madaktari bingwa kushoto ni Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajabu Abdurhamani akizungumza wakati wa ziara hiyo kulia ni Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani akizungumza mara\ baada ya ziara hiyo kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajabu Abdurhamani
Mkurugenzi Msaidizi kutoka Hospitali ya Benjamini Mkapa ya Jijini Dodoma Dkt Henry Humba ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu

Na Mwandishi Wetu,Tanga.

CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga kimesema kwamba kinaridhishwa na utendaji mzuri wa madaktari katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo katika utoaji wa huduma kwa wagonjwa kuliko ilivyo kuwa miaka ya nyuma.

Akizungumza leo wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ziara ya Kamati ya Siasa Mkoa wa Tanga kutembelea Kambi ya Matibabu ya Madaktari Bingwa kutoka Hospitali ya Benjamini Mkapa Dodoma walioweka kambi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajab Abdurhaman alisema kwa sasa huduma zimeboreshwa kwa kiwango kikubwa.

Alisema kwamba hivi sasa madaktari walikuwa wakijituma na kufanya kazi kwa ueledi mkubwa katika kuhakikisha wana wahudumia wagonjwa ambao wanakwenda kupata huduma hatua ambayo imepunguza kwa asilimia kubwa malalamiko.

"Nikiri Hospital ya Bombo sio ile tulioku tunaifikia zamani sasa hivi imebadilika sana kwa huduma maana yale malalamiko kwa wananchi yamepungua kwa asilimia kubwa na hata huduma zinazotewa wanaridhika nazo kwa kiasi kikubwa na madaktari wamekuwa msaada mkubwa kwao "Alisema Mwenyekiti huyo

Mwenyekiti huyo alisema kwamba wanamshukuru Rais Samia Suluhu kwa kuboresha huduma katika Hospitali hiyo ikiwemo ununuzi vifaa vya kisasa vilivyopo kwa ajili ya uchunguzi ikiwemo Cstan ambavyo zamani havikuwep

Alisema kwamba ametembelea kambi hiyo na kujionea namna madaktari wanavyo wahudumia wagonjwa na hivyo kulazimika kutoa pongezi kwao na wale waliopo kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo.

Sambamba na hayo lakini amewapongeza madaktari bingwa waliotoka Hospitali ya Benjamini Mkapa kuja kuungana na madaktari bingwa waliopo kwenye Hospitali hiyo kutoa huduma za kibingwa kwa wananchi

Aidha alisema wao kama watu waTanga wanawapongeza sana kwa maana kazi ya daktari na muuguzi ni wito hivyo mwenyezi Mungu atawalipa kwa yale yote mema mnayoendele kuwatendea watu wa Mkoa huo

"Tunampongeza Mbunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu kwa sababu yeye ni sehemu ya kuchangia jambo hilo kwa asilimia kubwa madkatri wafika hapo kutoa huduma za za afya kwa wananchi wa Mkoa na mungu ambariki sana kwa juhudi zake hizi" Alisema

Hata hivyo alisema pia wanamshukuru Rais Samia Suluhu ruhusa yake alitoa baada ya Mbunge Ummy kumuomba na kumruhusi jambo hilo kuendelea.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments