MAMA AUA MTOTO WAKE WA MIAKA 9



Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya, linamshikilia Regina Issack (40), anayedaiwa kuwa na matatizo ya akili, mkazi wa Ilindi, Kata ya Ilemi jijini Mbeya kwa tuhuma za mauaji ya mtoto wake, Sisela Ngailo (09).

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP, Benjamin Kuzaga amesema tukio hilo limetokea Februari 23, 2023 majira ya saa 7:00 mchana ambapo Regina alimnyonga shingo mwanae akiwa amelala.

"Chanzo cha tukio hili inasadikika mtuhumiwa kuwa na tatizo la afya ya akili ambapo alikuwa akihudhuria matibabu ya afya katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (MZRH) tayari uchunguzi wa tukio hili unaendelea na mtuhumiwa atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika," amesema Kamanda Kuzaga.

CHANZO - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments