SIMBA SC YAANZA VIBAYA HATUA YA MAKUNDI CAFCL, YACHAPWA 1-0 HOROYA AC


***************************

NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya Simba imeshindwa kutamba katika mchezo wake wa kwanza hatua ya makundi katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika baada ya kuambulia kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Horoya AC ya nchini Guinea.

Horoya AC ilianza kupata bao kupitia kwa nyota wao kutoka nchini Senegal, Pape Ndiaye aliefunga kwa kichwa dakika ya 18 kipindi cha kwanza.

Katika mchezo huo licha ya kipindi cha kwanza Horoya AC kutawala mchezo, kipindi cha pili Simba walirudia na hali ya kutaka kurudisha bao na kuweza kupata ushindi kwenye mchezo huo lakini matumaini yakayeyuka baada ya Nahodha wao John Bocco kukosa nafasi nyingi za wazi.

Kwenye mchezo huo ambao ulipigwa katika dimba la Lansana Conte General nchini Guinea, Aishi Manula alionesha umwamba wake kwa kuchomoa penati ambayo ilisababishwa na Josh Onyanga kuushika mpira ndani ya boksi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments