EWURA YAIBUKA KIDEDEA UHUSIANO MZURI NA VYOMBO VYA HABARI, KAGUO MTENDAJI BORA


Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imeibuka mshindi wa kwanza kwa Taasisi zenye uhusiano mzuri na vyombo vya habari, TRA imeshika number mbili na CRDB imekuwa ya tatu, Tuzo hiyo imetolewa leo Tar.18/02/2023 na Chama cha Maafisa Uhusiano Tanzania, Dar es Salaam.

Sambamba na hilo pia Meneja wa Mawasiliano EWURA, Bw. Titus Kaguo, ameibuka kuwa mtendaji bora wa Mawasiliano na Uhusiano katika sekta ya mafuta na gesi Tanzania.

Tuzo hizo zimefunguliwa na na Naibu Waziri wa Habari, Mhe. Kundo Mathew na kuhudhuriwa na Wataalamu wa Habari na Mawasiliano wa Serikali na sekta binafsi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments