AKAMATWA NA KOBE 998 AKIDAI WANATIBU UKIMWI



Mwanaume mmoja mkazi wa Kijiji cha Nyarukoru, mkoani Mara, Matimba Washa (28), amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Butiama kwa makosa matatu likiwemo kukutwa na kobe 998, magamba 10 ya kobe, ngozi ya Nyati na mkia wa Nyumbu, vyenye jumla ya thamani ya TZS milioni 168.


Katika mahojiano yake na Polisi mshitakiwa amedai kuwa ameoteshwa na mapepo kuwa nyara hizo za Serikali ni tiba ya magonjwa kama vile UKIMWI, Selimundu na magonjwa mengine ya zinaa hivyo kuwaomba wamletee mtu yeyote mahakamani hapo mwenye ugonjwa mmojawapo ili awathibitishie uwezo wa dawa hizo.


Mwendesha mashtaka, Wakili wa Serikali Gaston Kayombo amesema mshitakiwa huyo anashitakiwa kwa makosa matatu ya kukutwa na nyara za serikali pamoja na uhujumu uchumi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments