RAIS WA PAP CHIFU CHARUMBIRA ASHIRIKI IBADA YA JUMAPILI KANISA LA ZCC RAYTON PRETORIA, APONGEZA VIONGOZI WA DINI KUHAMASISHA AMANI NA UMOJA


Rais wa Bunge la Afrika (Pan African Parliament PAP) Mhe. Chifu Fortune Charumbira ameshiriki Ibada ya Jumapili leo Novemba 6, 2022 katika Kanisa la Zion Christian Church (ZCC) lililopo Mbungo 2 Rayton, Pretoria nchini Afrika Kusini.

Akihutubia maelfu ya waumini wa Kanisa la Zion Christian Church (ZCC) kwenye Ibada iliyoongozwa na Askofu Dkt. Nehemiah Mutendi, Mhe Chifu Fortune Charumbira amewapongeza viongozi wa dini kwa jukumu muhimu wanalofanya katika kukuza umoja duniani kote huku akibainisha kuwa Bunge la Afrika linatambua jukumu muhimu ambalo kanisa linachukua katika kushughulikia migogoro katika kutafuta amani na maendeleo duniani.


“ZCC imedhihirisha kuwa ni kanisa la dunia nzima, si la nchi flani, kwenye Ibada hii kuna watu kutoka nchi mbalimbali kwenye mkusanyiko huu wa kanisa. Askofu Nehemiah Mutendi ana mikutano mikubwa katika mabara yote. Bunge la Afrika linaamini kuwa ili kuwa amani na utatuzi wa migogoro lazima tumtangulize mbele Mwenyezi Mungu. Ulimwengu wa kiroho hufundisha watu kuwa waaminifu na kupiga vita ufisadi. Kadiri watu wanavyojiunga na kanisa ndivyo matatizo mengi kama vile migogoro na njaa yanavyotatuliwa", amesema Chifu Charumbira.
Askofu wa Kanisa la ZCC Dkt. Nehemiah Mutendi akimkaribisha Rais wa Bunge la Afrika (PAP) Mhe. Chifu Fortune Charumbira (kulia) katika kanisa la ZCC.
Rais wa Bunge la Afrika (PAP) Mhe. Chifu Fortune Charumbira (kushoto) akiwa katika Kanisa la Zion Christian Church (ZCC) lililopo Mbungo 2 Rayton, Pretoria nchini Afrika Kusini.
Rais wa Bunge la Afrika (PAP) Mhe. Chifu Fortune Charumbira (kushoto) akiwa katika Kanisa la Zion Christian Church (ZCC) lililopo Mbungo 2 Rayton, Pretoria nchini Afrika Kusini.


Rais wa Bunge la Afrika (PAP) Mhe. Chifu Fortune Charumbira akizungumza katika Kanisa la Zion Christian Church (ZCC) lililopo Mbungo 2 Rayton, Pretoria nchini Afrika Kusini.
Waumini wakiwa katika Kanisa la Zion Christian Church (ZCC) lililopo Mbungo 2 Rayton, Pretoria nchini Afrika Kusini.
Waumini wakiwa katika Kanisa la Zion Christian Church (ZCC) lililopo Mbungo 2 Rayton, Pretoria nchini Afrika Kusini.
Waumini wakiwa katika Kanisa la Zion Christian Church (ZCC) lililopo Mbungo 2 Rayton, Pretoria nchini Afrika Kusini.
Waumini wakiwa katika Kanisa la Zion Christian Church (ZCC) lililopo Mbungo 2 Rayton, Pretoria nchini Afrika Kusini.
Waumini wakiwa katika Kanisa la Zion Christian Church (ZCC) lililopo Mbungo 2 Rayton, Pretoria nchini Afrika Kusini.
Waumini wakiwa katika Kanisa la Zion Christian Church (ZCC) lililopo Mbungo 2 Rayton, Pretoria nchini Afrika Kusini.


Waumini wakiwa katika Kanisa la Zion Christian Church (ZCC) lililopo Mbungo 2 Rayton, Pretoria nchini Afrika Kusini.

Rais wa Bunge la Afrika (PAP) Mhe. Chifu Fortune Charumbira (katikati) akiwa na viongozi mbalimbali wa dini katika Kanisa la Zion Christian Church (ZCC) lililopo Mbungo 2 Rayton, Pretoria nchini Afrika Kusini.


Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments