EWURA YAENDESHA SEMINA KWA MAFUNDI UMEME KANDA YA ZIWA...DC MBONEKO ATAKA UBORA WA HUDUMA 'UMEME USILETE MADHARA KWA WANANCHI'


Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza wakati akifungua Semina kwa Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza iliyoandaliwa na EWURA. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
 Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza wakati akifungua Semina kwa Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza iliyoandaliwa na EWURA. Kushoto ni Meneja wa EWURA Kanda ya Ziwa, George Mhina, kulia ni Mhandisi Mwandamizi wa Umeme kutoka EWURA, John Kitonga.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeendesha Semina kwa Mafundi Umeme mikoa ya Kanda ya Ziwa (Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza) kwa lengo la kuwaongezea uelewa wa masuala ya kiudhibiti hususani katika ufungaji wa mifumo ya umeme na namna bora ya kufanya kazi zao ili kuhakikisha huduma zinakuwa salama, bora na zilizofanyika kwa viwango vinavyokubalika.

Semina hiyo ya siku mbili imeanza leo Jumatano Oktoba 12,2022 katika ukumbi wa Shy Park Hotel Mjini Shinyanga ikihudhuriwa pia na maafisa kutoka VETA, TEMESA na TANESCO.

Akifungua Semina hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dk. Sophia Mjema, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko amesema kazi zinazofanywa na wadau wa fani ya ufungaji mifumo ya umeme ni za muhimu sana katika ustawi wa uchumi wa nchi hivyo zinapaswa kufanywa kwa weledi wa hali ya juu ili kulinda usalama wa maisha ya watu na mali zao.

“Kwa sababu kazi za umeme zinaweza kuleta madhara ikiwa zitafanywa chini ya kiwango ama kufanywa na fundi asiye na utaalamu huo, inaelekezwa kufanywa na mwenye utaalamu na aliyethibitishwa na Mamlaka kwa kupewa Leseni. Hivyo haipaswi kutumia leseni ya mtu mwingine kufanya kazi za umeme nan i kosa linaloweza kuadhibiwa kisheria”,amesema Mboneko.


“TANESCO hakikisheni mnatumia mafundi umeme waliosajiliwa na wenye leseni ili kuondoa vishoka wanaoharibu kazi na kusababisha majanga ya moto kutokana ufungaji umeme mbovu. Hatutaki kuona mtu asiye na leseni na hajasajiliwa anafanya kazi ya kuunganisha umeme. Hawa Vishoka wanaharibu sifa za mafundi umeme wenye vigezo”,ameongeza.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza kwenye Semina kwa Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza iliyoandaliwa na EWURA

Mkuu huyo wa wilaya amesema lengo la serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan ni kufikisha huduma ya umeme kwa wananchi ambao hauleti madhara kwa wananchi hivyo kuwataka wafundi umeme kuzingatia sheria za sekta ya umeme.

“Tunataka kuona umeme unaopelekwa kwa wananchi hauleti madhara kwa wananchi.Hatutakubali kuona wafundi wasiosajiwa na wasio na leseni wanafanya kazi ya kufunga umeme iwe majumbani, viwandani ama sehemu za biashara. Tunataka kuona ubora wa kazi ili kuondokana na lawama”,amesema Mboneko.

Kwa upande wake Meneja wa EWURA, George Mhina amesema EWURA imeamua kutoa semina kwa mafundi umeme kwa lengo la kuwaongezea uelewa wa masuala ya kiudhibiti hususani katika ufungaji wa mifumo ya umeme na kuwajengea uwezo wa namna bora ya kufanya kazi ili kuhakikisha huduma wanazotoa zinakuwa salama,bora na zilizofanyika kwa viwango vinavyokubalika ili kuepuka majanga ya moto.

Mhina ameeleza kuwa, mwaka 2008, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha Sheria ya Umeme “Electricity Act” na kifungu namba 8 (h) cha sheria hiyo kinaelekeza kazi zote za ufungaji wa mifumo ya umeme (majumbani,viwandani ama sehemu za biashara) zifanywe na mtaalamu aliyeomba na kupewa leseni na mamlaka husika ambayo ni EWURA.

“Lengo kuu la kudhibiti huduma za ufungaji wa mifumo ya umeme ni kuhakikisha kazi hiyo inafanywa kitaalamu na wale tu wenye ujuzi na weledi katika fani ya umeme ili kumhakikishia mtumiaji wa huduma hizo usalama na ubora wa huduma”,amesema Mhina.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza wakati akifungua Semina kwa Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza iliyoandaliwa na EWURA leo Jumatano Oktoba 12,2022 Mjini Shinyanga. Kushoto ni Meneja wa EWURA Kanda ya Ziwa, George Mhina. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza wakati akifungua Semina kwa Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza iliyoandaliwa na EWURA.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza wakati akifungua Semina kwa Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza iliyoandaliwa na EWURA.
Meneja wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Ziwa, George Mhina akizungumza kwenye Semina kwa Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza iliyoandaliwa na EWURA. Katikati ni ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akifuatiwa na Mhandisi Mwandamizi wa Umeme kutoka EWURA, John Kitonga. 
Meneja wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Ziwa, George Mhina akizungumza kwenye Semina kwa Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza iliyoandaliwa na EWURA. Katikati ni ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akifuatiwa na Mhandisi Mwandamizi wa Umeme kutoka EWURA, John Kitonga. 
Meneja wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Ziwa, George Mhina akizungumza kwenye Semina kwa Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza iliyoandaliwa na EWURA. Katikati ni ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akifuatiwa na Mhandisi Mwandamizi wa Umeme kutoka EWURA, John Kitonga. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akimpatia Cheti na Leseni fundi umeme, Charles Jackson. Wa kwanza kushoto Meneja wa EWURA Kanda ya Ziwa, George Mhina wa pili kulia ni Mhandisi Mwandamizi wa Umeme kutoka EWURA, John Kitonga. 
Meneja wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Ziwa, George Mhina akitoa elimu kwa Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza iliyoandaliwa na EWURA
Meneja wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Ziwa, George Mhina akitoa elimu kwa Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza iliyoandaliwa na EWURA
Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa na EWURA
Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa na EWURA

Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa na EWURA
Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa na EWURA
Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa na EWURA
Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa na EWURA
Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa na EWURA
Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa na EWURA
Maafisa kutoka TANESCO Shinyanga wakiwa kwenye semina kwa Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza  iliyoandaliwa na EWURA

Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa na EWURA
Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza wakiwa kwenye semina iliyoandaliwa na EWURA
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko maafisa kutoka EWURA,TEMESA wakipiga picha ya pamoja na Mafundi Umeme mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko maafisa kutoka EWURA,TEMESA wakipiga picha ya pamoja na Mafundi Umeme mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko maafisa kutoka EWURA,TEMESA wakipiga picha ya pamoja na Mafundi Umeme mkoa wa Mwanza.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko maafisa kutoka EWURA,TEMESA wakipiga picha ya pamoja na Mafundi Umeme mkoa wa Geita
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko maafisa kutoka EWURA,TEMESA wakipiga picha ya pamoja na Mafundi Umeme mkoa wa Simiyu.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko maafisa kutoka EWURA,TEMESA wakipiga picha ya pamoja na maafisa kutoka taasisi mbalimbali mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko maafisa kutoka EWURA,TEMESA wakipiga picha ya pamoja na wafanyakazi wa EWURA.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments