JINSI YA KUGUNDUA KAMA MTOTO WAKO ANA KIPAWA


Suala la kwamba mtoto anaweza kuwa na zawadi ya kipaji ni jambo ambalo wakati mwingine linaweza kupingwa.

Kwa upande mmoja, wanasayansi wa neva pamoja na wanasaikolojia na wengine wanasema kwamba watoto pekee wana mgao wa akili (IQ) ambayo ni zaidi ya inavyopaswa kuwa, kuwa nayo ni zawadi kubwa.


Kwa upande mwingine, wananadharia wa elimu pamoja na wale wanaotoa mafunzo ya michezo, wanasema kuwa Zawadi ya aina hii ni hatua kubwa, na pia wanasema kwamba watoto wana akili katika baadhi ya mambo tofauti.


Mjadala kuhusu mada hii bado unaendelea kwa muda mrefu.

Lakini kuna makubaliano kwamba watoto wanaofanya mtihani wa IQ ili kujua kiwango chao cha akili wana vipawa vya angalau asilimia 97.


Kwa mfano, huko Brazili, Theo Costa Ribeiro ni mtoto mwenye umri wa miaka sita kutoka jiji la Sao Paulo, ambaye ana zawadi ya hekima.


Alianza kuzungumza akiwa na umri wa miezi sita tu, na alipokuwa na umri wa mwaka mmoja na miezi sita tu, alianza kusema kwa sentensi na kuanza kwenda shule.


Ygor Ribeiro, babake Theo, anasema kwamba "aliona neno moja na akatuuliza maana ya neno hilo, kwa maneno mengine, lakini maswali hayo hayakuwa maswali ya kijinga."


Ygor aliambia BBC kwamba familia yake haikumlazimisha Theo kujifunza chochote, wala hawakupuuza maswali yake.


Wakati Theo alipokuwa na umri wa miaka mitatu, alikuwa tayari kusoma, kuandika na kufanya hisabati.


Walimu walikuja na kuwataka wazazi wake wampime IQ, kwa sababu alionyesha akili nyingi kuliko wenzake.


Jaribio hilo lilionyesha kuwa Theo, ambaye wakati huo alikuwa na umri wa miaka mitano, alikuwa na akili ya mtoto wa miaka 14-15.


Hii haimaanishi kuwa haishi kama mtoto. Anapenda kupata marafiki wapya, anapenda kucheza michezo, michezo ya harakati na anapenda kucheza na watoto wa umri wake.


Utagunduaje kwamba mwanao ana kipawa?


Kwa kuanzia, ingawa ni kiashiria kizuri, kwamba mtoto mwenye akili ya juu haimaanishi kuwa ana kipawa, inajulikana haswa baada ya kukamilika kwa vipimo mbalimbali, haswa IQ ambayo hufanywa kuelewa asili ya ubongo.


Wanasaikolojia wa neva /au wanasaikolojia na wataalamu katika nyanja hii hufanya utafiti huu.


Haya ni mambo ambayo Sekretarieti ya Elimu Maalum ya MEC (2006) inabainisha mambo yanayoweza kuashiria kuwa mtoto wako amejaaliwa:



Udadisi
Misamiati zaidi ya wenzake
Mwanafunzi anayeshika haraka na uwezo wa juu wa kiakili
Kufikiri kwa haraka
Kuwa kiongozi na kujiamini
Kukumbuka mambo haraka
Kuwa mbunifu
Uwezo wa kurekebisha au kubadilisha mawazo yake
Kuchunguza siri
Jitahada za kupata anachotafuta
Mtoto anaandika kwenye kompyuta



Kwa upande mwingine, kuna watoto ambao wana zawadi ya hekima ambayo hawajui kama wanayo.


Wakati fulani hawapendi kwenda shule, wakati mwingine wana matatizo ya kitabia.


"Kuna watu wengi wenye vipawa ambao hawafanyi vizuri shuleni kwa sababu hawana nia ya kujifunza, na kwa sababu hakuna kitu cha kusisimua akili zao, shuleni wamechoka na hawaboreshi kile wanachoweza kufanya," alisema Fabiano de Abreu , daktari katika uwanja wa 'sayansi ya neva'.

Chanzo - BBC Swahili

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments