SERIKALI KUANDAA KANUNI ZA UDHIBITI WA BEI YA DAWA NA VIFAA TIBA


********************

Na WAF, Bungeni, Dodoma.

Serikali ipo mbioni kuandaa kuani za kudhibiti bei za dawa nchini na tayari rasimu ya kanuni hizo zimeshawasilishwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Godwin Mollel alipokuwa akijibu swali lilioulizwa na Mheshimiwa. Mhandisi Mwanaisha Ng’anzi Ulenge (Mbunge Viti Maalum) Bungeni, Jijini Dodoma.

Mhe. Ulenge amehoji Serikali ina mpango gani wa kutoa bei elekezi ya vifaa vya tiba haswa akilenga vya macho, pua na koo.

Akijibu Kuhusu Vifaa tiba, Dkt. Mollel amesema kuwa bei elekezi za vifaatiba zitaandaliwa mara tuu baada ya kukamilika kwa kanuni za bei za dawa elekezi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments