SIRI YA KUTOZEEKA MAPEMA


Mtu mwenye umri mkubwa zaidi duniani, Kiko Tanaka, alifariki akiwa na na umri wa miaka

Hapo zamani, maisha marefu yalionekana ni kitu kisichowezekana. Lakini sasa mambo yamebadilika. Je uzee kucheleweshwa au hata kuzuiwa? Je wale wenye umri wa zaidi ya miaka 100 wanasiri ambayo inaweza kumsaidia kula mtu kuishi miaka mingi?.


Ijumaa,Januari 2, 1903, mtoto mchanga wa kike anayeitwa Kiko Tanaka alizaliwa katika kijiji kidogo kilichopo katika kisiwa cha kusini mwa Japan. Katika mwaka huo huo, mashindano yam bio za baiskeli ya Tour de France yalianzishwa Paris na kampuni ya magari ya Ford iliuza gari lake la kwanza. Kiko Tanaka alifariki dunia Aprili akiwa na umri wa miaka 119, na alitambuliwa rasmi kama mtu mwenye umri mkubwa zaidi duniani.


Aliishi miaka yake ya mwisho ya maisha yake katika nyumba ya wazee, akiamka saa kumi na mbili asubuhi kila siku kufanya hesabu, kucheza michezo ya ndani ya nyumba, kula chokoleti na kunywa kahawa na soda.


Kuwapata watu wanaoishi miaka zaidi ya mia moja kama Koshi Tanaka sasa sio jambo lisilo la kawaida.

Chanzo - BBC SWAHILI

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments