YANGA YAUA MNYAMA SIMBA....YATINGA FAINALI KUBABE


NA EMMANUEL MBATILO

Rasmi, Klabu ya Yanga Sc yatinga hatua ya fainali kombe la Azam Federation Cup mara baada ya kuwanyuka mahasimu wao Simba Sc kwa bao 1-0 mchezo uliopigwa kwenye dimba la CCM Kirumba Mwanza.

Bao la Yanga Sc limewekwa kimyani na kiungo matata Feisal Salumu ‘Fei Toto kwa shuti kali lililomshinda mlinda lango Beno Kakolanya na kutinga fainali.

Yanga Sc sasa wanawasubiri kati ya Azam Fc ama Coastal Unions ambao watauma hapo kesho katika dimba la Amri Abedi Jijini Arusha.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments