WALIOFUKUZWA CHADEMA WAINGIA BUNGENI




Baadhi ya wabunge hao ni Esther Matiko na Salome Makamba

Baadhi ya Wabunge wa Viti Maalum waliofukuzwa uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) juzi Ijumaa Mei 13, 2022, wameudhuria vikao vya Bunge na kuuliza maswali isipokuwa Mhe.Halima Mdee na Mhe.Ester Bulaya.

Baadhi ya wabunge hao waliingia ndani ya Bunge kwa nyakati tofauti huku Mhe.Ester Matiko, akiwa wa kwanza kuingia akifuatiwa na Mhe.Salome Makamba na wengine waliingia baadaya kikao cha Bunge kuanza huku wengine wakiingia baada ya Bunge kuanza.

Kila mmoja ameingia na wakati wake, tofauti na mara ya kwanza walipofika kwa ajili ya kuapishwa ambapo waliingia wote 19 katika viwanja vya Bunge.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments