RAIS SAMIA AZINDUA NEMBO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwenye kukata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Nembo ya Sensa ya Watu na Makazi ambapo itaanza kutumika baada ya kutangaza kuwa Sensa hiyo itafanyika tarehe 23 Agosti 2022 nchi nzima. Hafla ya uzinduzi huo imefanyika leo tarehe 08 April 2022 mjini Zanzibar.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Viongozi mbalimbali kabla ya kuzindua rasmi Nembo ya Sensa ya Watu na Makazi ambayo itaanza kutumika rasmi, baada ya kutangaza kuwa Sensa hiyo itafanyika tarehe 23 Agosti 2022 nchi nzima. Hafla ya uzinduzi huo imefanyika leo tarehe 08 April 2022 mjini Zanzibar.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, akikabidhi Nembo ya vyeti maalum kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. John Jingu, kuashiria kumpa Jukumu la kuanza kazi hiyo wakati wa uzinduzi rasmi wa Nembo ya Sensa ya Watu na Makazi ambapo Sensa hiyo itafanyika tarehe 23 Agosti 2022 nchi nzima. Hafla ya uzinduzi huo imefanyika leo tarehe 08 April 2022 mjini Zanzibar. Kushoto ni Rais wa Zanzibar Dkt. Hessein Ali Mwinyi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, akikabidhi Nembo ya vyeti maalum kwa Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ambae pia ni Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Sensa, kuashiria kumpa Jukumu la kuanza kazi hiyo rasmi wakati wa uzinduzi rasmi wa Nembo ya Sensa ya Watu na Makazi ambayo itaanza kutumika, baada ya kutangaza kuwa Sensa hiyo itafanyika tarehe 23 Agosti 2022 nchi nzima. Hafla ya uzinduzi huo imefanyika leo tarehe 08 April 2022 mjini Zanzibar.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments