SIMBA SC YAJIPANGA KUICHAPA US GENDARMARIE NA KUTINGA ROBO FAINALI


*****************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KLABU ya Simba imeruhusiwa kuingiza mashabiki takribani 35,000 kwenye mchezo wake wa nyumbani wakiwakaribisha timu ya US Gendarmerie mchezo ambao utapigwa tarehe 03/04/2022 kwenye dimba la Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Simba Sc, Bw.Ahmed Ally amesema tiketi tayari zinauzwa mitandaoni na kwa mashabiki wetu waliopo mikoani hakuna haja ya kununua tiketi hadi wakifika Dar es Salaam.

"Tumeruhusiwa mashabiki 35,000. Awali tuliomba kuongeza idadi ya mashabiki kupitia kwa TFF lakini kwa sababu ya mambo ya Covid wameruhusu idadi ya mashabiki 35,000. Mashabiki ambao wanataka kuja kuona mchezo wanunue tiketi mapema." Amesema Bw.Ahmed Ally

Amesema wataingia kwenye mchezo wa jumapili wakiwa na lengo moja ushindi na wanaimani watashinda na kutinga hatua ya robo fainali.

Aidha amesema siku ya jumatano watakuwa standi ya Magufuli watakuwa pale kwa pamoja na mgeni wetu rasmi atakuwa ni Mwenyekiti wa klabu, Murtaza Mangungu.

"Tukio letu la jumatano kwenye stendi ya Magufuli itakuwa saa 4 hadi 5 asubuhi. Tunakutana pale kufurahi, kushangilia Simba yetu". Amesema Ahmed Ally.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments