UCSAF YAKUTANA NA WADAU WA MAWASILIANO KANDA YA ZIWA...MKUU WA TCRA ATAKA WAPENDANE

Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) akifungua Mkutano wa wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa leo Jumanne Faberuari 15,2022 katika Ukumbi wa BoT Jijini Mwanza
*****

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) umekutana na Wadau wenye Leseni za huduma za mawasiliano Kanda ya Ziwa kwa lengo la kutoa elimu inayohusu majukumu ya UCSAF pamoja na haki na wajibu wa watoa huduma za maudhui kwa njia ya Televisheni, Redio, Mitandao ya Kijamii na wasambaji wa maudhui kwa njia ya waya (CATV).

Akifungua Mkutano wa wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa leo Jumanne Februari 15,2022 Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) amewataka watoa huduma za mawasiliano kupendana na kuacha ubinafsi.

“Mkiacha huu wivu usio na manufaa kwenye hizi Redio zenu mtafika mbali, Mpendane kama kuna shida njoo TCRA tuzungumze,tumieni mnara mmoja ili kupunguza gharama za uendeshaji. Acheni kuchongeana…Hivi Redio ya mwenzako ikizimwa wewe utafaidika nini?”,amesema Mhandisi Mihayo.


Aidha amehamasisha watoa huduma za mawasiliano kwa njia ya redio kuongeza usikivu akibainisha kuwa nafasi za kuongeza usikivu wa Redio kwenye maeneo mbalimbali zipo na TCRA inaendelea kuzitoa.

“TCRA inataka kuwe na Redio kila mahali kwa sababu usikivu wa redio upo chini ya asilimia 50. Nafasi za kuongeza usikivu bado zipo, njooni TCRA tuwapatie lakini pia napenda kuwataarifu kuwa ukianzisha Redio Tozo zimepungua kwani serikali inataka kila mahali kuwe na redio. Nami nataka kuona Kanda ya Ziwa inaongoza kuwa na watoa huduma wengi wa mawasiliano”,amesema Mhandisi Mihayo.

Afisa Sheria Mwandamizi wa UCSAF, Fredy Kandonga amesema UCSAF inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ukiwemo wa Mawasiliano ya simu ili kufikisha huduma za mawasiliano katika maeneo yasiyo na huduma hiyo na yenye mawasiliano hafifu, kuboresha usikivu wa redio ya Taifa na Redio za Kijamii, Uanzishwaji wa kituo cha miito ya dharura, Tiba Mtandao, Kuunganisha shule kwenye Intaneti na Mafunzo ya TEHAMA kwa walimu.

Amesema wajibu wa mfuko huo ni pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa uunganishwaji wa kila mtu kwenye mitandao ya mawasiliano ya umma kupitia huduma za mawasiliano ,kuhakikisha huduma za posta na matangazo zinapatikana maeneo ya vijijini na mijini yenye huduma za mawasiliano hafifu na kubainisha na kuainisha maeneo yanayohitaji huduma za mawasiliano kwa wote.

Ameongeza kuwa Wajibu wa watoa huduma ni kushiriki katika upelekaji wa huduma za mawasiliano kwenye maeneo ya vijijini na mijini yasiyo na huduma au yenye huduma hafifu pamoja na kutoa tozo ya huduma kwa wote kila robo mwaka.

TAZAMA PICHA HAPA CHINI
Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) akifungua Mkutano wa wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa leo Jumanne Faberuari 15,2022 katika Ukumbi wa BoT Jijini Mwanza. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) akifungua Mkutano wa wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa leo Jumanne Faberuari 15,2022 katika Ukumbi wa BoT Jijini Mwanza
Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) akifungua Mkutano wa wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa leo Jumanne Faberuari 15,2022 katika Ukumbi wa BoT Jijini Mwanza
Mwanasheria wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) Fredy Kandonga akizungumza wakati wa Mkutano wa wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa leo Jumanne Faberuari 15,2022 katika Ukumbi wa BoT Jijini Mwanza
Mwanasheria wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) Fredy Kandonga akizungumza wakati wa Mkutano wa wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa leo Jumanne Faberuari 15,2022 katika Ukumbi wa BoT Jijini Mwanza
Mwanasheria wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) Fredy Kandonga akizungumza wakati wa Mkutano wa wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa leo Jumanne Faberuari 15,2022 katika Ukumbi wa BoT Jijini Mwanza
Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) akisisitza jambo kwenye Mkutano wa wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa. Kushoto ni Mwanasheria wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) Fredy Kandonga .
Mwanasheria wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) Fredy Kandonga akizungumza kwenye Mkutano wa wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa. Kulia ni Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF).
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) leo Jumanne Faberuari 15,2022 katika Ukumbi wa BoT Jijini Mwanza
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) leo Jumanne Faberuari 15,2022 katika Ukumbi wa BoT Jijini Mwanza
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye mkutano ulioandaliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakipiga picha ya kumbukumbu
Wadau wa mawasiliano Kanda ya Ziwa wakipiga picha ya kumbukumbu

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments